Thursday, May 27, 2021

KATIBU MKUU KILIMO ANDREW MASSAWE AIAGIZA CPB KUSHIRIKIANA NA NFRA ILI KURAHISISHA UPATIKANAJI WA MASOKO YA MAZAO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa  Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza ili kujionea utekelezaji wa majukumu unaofanywa na Bodi hiyo katika Ofisi za Kanda Jijini Dodoma, Tarehe 27 Mei 2021. (Picha Zote Na Mathias Canal)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa  Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza ili kujionea utekelezaji wa majukumu unaofanywa na Bodi hiyo katika Ofisi za Kanda Jijini Dodoma, Tarehe 27 Mei 2021.
Sehemu ya washiriki wakifatilia maelekezo ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe akisisitiza jambo wakati alipotembelea  Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) katika Ofisi za Kanda Jijini Dodoma, Tarehe 27 Mei 2021.
Sehemu ya washiriki wakifatilia maelekezo ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe akisisitiza jambo wakati alipotembelea  Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) katika Ofisi za Kanda Jijini Dodoma, Tarehe 27 Mei 2021.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa  Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza ili kujionea utekelezaji wa majukumu unaofanywa na Bodi hiyo katika Ofisi za Kanda Jijini Dodoma, Tarehe 27 Mei 2021.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma


Bodi ya nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) imeagizwa kushirikiana na Taasisi zingine za Serikali ikiwemo Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) katika kuimarisha upatikanaji wa masoko ndani na nje ya nchi.


Agizo hilo limetolewa tarehe 27 Mei 2021 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Ndg Andrew Massawe wakati alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko kwa lengo la kufahamiana, na kuzungumza na Menejimenti ikiwa ni kufuatilia utekelezaji wa majukumu unaofanywa na Bodi hiyo katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya masoko kwa mazao ya wakulima nchini.

 

Massawe amesema kuwa CPB na NFRA zinapaswa kuwajibika ipasavyo katika kununua na kuuza mazao ya wakulima ndani na nje ya nchi kwani kufanya hivyo kutaongeza wigo wa masoko ya mazao ya wakulima.


Ameitaka CPB kujiimarisha zaidi katika kununua na kuuza mazao ya wakulima ikiwa ni pamoja na kuhakikisha gharama za uendeshaji (operational cost) zinakuwa ndogo, na kwà kufanya hivyo Taasisi itapata faida na mkulima atapata manufaa Kwà mazao yake kuwa na uhakika wa soko.


Katibu Mkuu Massawe amewataka watendaji CPB kutumia muda wao wote wanapokuwa kazini kufikiri kibiashara kwani Bodi hiyo ni maalumu kwa mujibu wa sheria kwa ajili ya kufanya biashara ya mazao.


Katika hatua nyingine Katibu Mkuu Massawe ameagiza watumishi wote wa Taasisi hiyo kuwajibika ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuonyesha ushirikiano maradufu kwani kumekuwa na sintofahamu baini yao kwa kuchukiana wenyewe kwa wenyewe.


Amesema CPB inapaswa kuimarisha na kuwa na mahusiano mazuri ya kikazi kwani utekelezaji wa majukumu ya ufanyaji biashara wanayoifanya inahitaji mahusiano mazuri baina yao.


“Hapa ndani nasikia mnavurugana sana, hamuwezi kufanya kazi kwa mafanikio kama hakuna maelewano, Maneno yanakuwa mengi kwanini mnavurugana kwani shida nini ambacho hakizungumziki, Nawasihi Mkae meza moja na kuzungumza kwanini taasisi inakuwa na ugomvi na kutokuelewana” Amekaririwa Katibu Mkuu Massawe


Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Dkt Anslem Moshi amekiri kuwepo kwa sintofahamu baina ya wafanyakazi na kumuhakikishia Katibu Mkuu huyo jambo hilo kulichukulia hatua za haraka iwezekanavyo.


MWISHO

No comments:

Post a Comment