Friday, November 30, 2018

Majaliwa akasirika wafanyabiashara Katoro kuchangishwa fedha

Na George Binagi-GB Pazzo

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, Novemba 30, 2018 amehitimisha ziara yake ya siku nne mkoani Geita kwa kuzungumza na wakazi wa Katoro akiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege Chato ambapo pamoja na mambo mengine alikasirishwa kusikia wafanyabiashara wamechangishwa fedha kwa ajili ya mafuta ya ukarabati wa barabara za mitaa.


Majaliwa alisisitiza kwamba serikali haitawavumilia baadhi ya watumishi wasio waadilifu ambao wanatafuna fedha za maendeleo ambapo akiwa katika wilaya ya Nyang’hwale aliagiza watumishi wote wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhilifu wa zaidi ya shilingi bilioni tatu wakamate na kuchukuliwa hatua za kisheria na tayari watumishi saba akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbogwe, Carlos Gwamagobe wamekamatwa kwa ajili ya uchunguzi kuhusiana na ubadhilifu huo.


Aidha akiwa wilayani Mbogwe, Majaliwa alimuagiza Mkuu wa Mkoa Geita, Mhandisi Robert Gabriel kumsimamisha kazi aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Mbogwe, Adam Nyoni ambaye amehamishiwa Halmashauri ya Nyang’hwale ili akajibu tuhuma za ubadhilifu wa shilingi milioni 19.4 za mfuko wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Tazama Video hapa chini

No comments:

Post a Comment