Friday, December 2, 2016

MBUNGE RIDHIWANI AWANGOZA WANANCHI KUPIMA VIRUSI VYA UKIMWI

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani akiwa katika  kituo cha kupima na kutoa Elimu ya gonjwa la Ukimwi kilichopo Mdaula, Chalinze akitolewa damu kwa ajili ya kupima virusi vya HIVvinavyosababisha Ukimwi jimboni humo ikiwa ni siku ya Ukimwi Duniani..
Baadhi ya wananchi wa jimbo la chalinze walijitokeza katika mkutano wa Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani mara baada ya kumaliza zoezi la upimaji virusi vya Ukimwi.
Mbunge akibadilishana na moja wa wazee maarufu katika kata ya Bwilingu Aliyejulikana kwa jina la Mzee Mbise , baada ya mkutano na wananchi.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Bwilingu Ndg. Saidi Khalfan akieleza jambo katika mkutano wa wananchi wa Kitongoji cha Bwilingu huku Mbunge akichukua maelezo ya wananchi hao na wa pili kutoka kushoto ni Diwani wa Kata ya Bwilingu Ndg. lufunga  wa kwanza kushoto  ni Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo Ndg. Hussein Mlamba.
Mbunge Ridhiwani akizungumza na wananchi walijitokeza kituoni hapo hawapo pichani katika siku ya Ukimwi Duniani

Katika zoezi hilo watu walijitokeza kupima wakiongozwa na Mbunge wao, watu watatu waligundulika kuwa na maambukizi  virusi vya HIV kati ya watu 81 waliojitokeza kupima..

No comments:

Post a Comment