Moja ya malori yaliyoteketezwa
Marekani
na Urusi zimelaumiana vikali kwenye baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa juu ya mashambulizi dhidi ya msafara wa misaada nchini Syria,
pamoja na hatua ya kuvunja mkataba wa kusitisha mapigano.
Wamarekani wamekuwa wakiamini kuwa Urusi ndio iliyoshambulia msafara huo, huku Warusi wakilipinga hilo.
Waziri wa
Mambo ya Nchi za Nje wa Urusi John Kerry, alitoka nje ya lugha ya
kidiplomasia kwa kutumia dhihaka zaidi. Huku mwenzake wa Urusi Sergey
Lavrov akipinga hisia hizo kali kwa kuorodhesha mifano kadhaa kutetea
nchi yake. Aidha ametaka pia kufanyika.
Licha ya
majibizano makali, Urusi na Marekani zilikubaliana kwa pamoja kuongoza
mkutano wa mataifa 23, yanayoiunga mkono Syria ambao utafanyika mjini
New York, baadaye leo.
Katika
hatua nyingine Umoja wa Mataifa umesema unajiandaa kuanza tena kutoa
misaada ya kibinadamu katika maeneo yaliyozingirwa nchini Syria, baada
ya kusitishwa kwa usambazaji wa misaada kufuatia shambulio hilo.
Mjumbe wa
Umoja wa Mnataifa nchini Syria, Staffan de Mistura ameiambia BBC kwamba
misafara hiyo ya misaada itaanza katika baadhi ya maeneo lakini kwa
uangalifu na tahadhari kubwa. Misaada hiyo amesema haitasambazwa katika
eneo linaloshikiliwa na waasi la Aleppo, ambalo limeshambuliwa vibaya. BBC
No comments:
Post a Comment