Na Hamisi Hussein – Singida
WALIMU Wakuu wa
shule za Msingi na Maafisa elimu ngazi ya Kata na Wilaya Mkoani Singida
wametakiwa kufanya tathmini ya hali utoaji elimu kwa wanafunzi hususani darasa
la saba na la nne mara kwa mara ili kubaini na kutatua changamoto zinazorudisha
nyuma ufundishaji na ujifunzaji jambo ambalo limepelekea kuwepo kwa mdororo wa
ufaulu.
Agizo hilo
limetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Daktari Fatuma Mganga wakati wa
kuwajengea uwezo Walimu wakuu, Maafisa Elimu hafla iliyofanyika katika shule ya
Mtakatifu Bernard ndani Manispaa ya Singida ambapo wawezeshaji kutoka Wilaya ya
Bahi Mkoani Dodoma ambayo wamekuwa wakifanya vizuri kwenye elimu Msingi.
Dk. Mganga
Amesema ni wakati sasa walimu hao pamoja na watendaji wengine wakiwemo maafisa
Elimu kutoka maofisi kwenda kwenye shule ambazo zinachangamoto ili kuinua hali
ya elimu kwa kufanya tathmini ya wanafunzi ambao wanashindwa kuwa na matokeo
mazuri.
“Twendeni Tukafanye kazi, tuache ubosi,
twendeni Tukafanye tathmini tujue mwanafunzi gani anachangamoto ipi ili tuweze kuzikabili
changamoto ambazo zinaturudisha nyumakiwango cha elimu kwenye mkoa wetu”.Alisema Dkt. Mganga
“Kiongozi unaweka mikakati ili kuweza
kuapata matokeo usisikilize Rumors tumia jitihada zako upate matokeo ili uweke
Legacy”. Aliongeza
Katibu Tawala huyo.
Dk Mganga
aliongeza kwa kusema kuwa viongozi wa Mkoa wa Singida wanapaswa kufanya kazi
kwa kujituma ili waweze kuweka alama hivyo akasisitiza walimu wakuu kujituma na
kujitoa Zaidi kwenye kutoa elimu kwa wanafunzi.
Afisa Elimu
Msingi Wilaya ya Bahi Boniface Willson ambaye alikuja kuwajengea uwezo walimu
wa mkoa wa Singida alisema kuwa mwaka 2017 Halmashauri ya Bahi ilikuwa na shule
ambazo zilikuwa hazifanyi vizuri kwenye elimu msingi hadi ikapewa bendera
nyeusi lakini baada ya kufanya tathimini kwa sasa imekuwa ikifanya vizuri.
Willson alisema
kujituma kwa walimu wakuu kwenye halmashauri hiyo ndiko kumeweza kubadilisha
kutoka ufaulu wa chini na sasa imekuwa moja ya halmashauri inayofanya vizuri ndani
Kimkoa hadi kitaifa.
Naye Mratibu wa
Programu ya Serikali ya Shule Bora Mkoa wa Singida Samweli Daniel amewashauri
wadau wa elimu wanapopanga mipango ya kuboresha elimu iwe inaandikiwa ripoti
ili zitumike wakati wa utekelezaji katika maeneo mbalimbali.
No comments:
Post a Comment