Wednesday, March 8, 2023

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA CHONGOLO UJENZI WA VITUO VYA POLISI MKALAMA NA IKUNGI

 

Waziri wa Mambo ya Ndani Mhandisi  Hamadi Masauni akiwa  anakagua jengo la Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama ikiwa ni utekelezaji wa Maagizo ya Katibu Mkuu wa CCM  Taifa
Kushoto kwake ni Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa. 




Waziri wa Mambo ya Ndani Mhandisi Hamad Masauni akikagua jengo la kituo cha Polisi Ikungi mapema hii leo Machi 8, 2023.




Gwaride la heshima kwa Waziri Mhandisi Masauni

Na Hamis Hussein - SINGIDA

WIZARA ya Mambo ya ndani ya Nchi imetekeleza maagizo ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa Daniel Chongolo ambaye alitaka kukamilishwa kwa ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Wilaya ya Ikungi na Mkalama ndani ya miezi mitatu ambavyo ujenzi wake ulikuwa umekwama kwa muda mrefu.

Hatua hiyo imejiri baada ya Waziri wa Mambo ya ndani Mhandisi Hamad Masauni kufika kukagua vituo hivyo vya Ikungi na Mkalama Leo Machi 8, 2023  ikiwa in ukelezaji wa maagizo hayo ambapo amesema katika mwaka huu wa fedha serikali imetenga Bilioni 1.1 kukamilisha kituo cha Polisi Ikungi na Milioni 476 kwajili ya Kituo cha Polisi Mkalama.

Mhandisi Masauni amesema serikali inaendelea kuboresha Mazingira ya Kazi kwa Polisi  ili wananchi wapate Huduma karibu na maeneno yao.

"Serikali chini ya Rais Samia imeendelea kuboresha Mazingira ya Polisi ambayo yanaokena kuwa Duni kupitia mradi wa kujenga vituo vya Polisi nchini"

"Tayari katika bajeti ya mwaka huu tumetenga Bilioni 1.1 kwajili kukamilisha Kituo cha Polisi Ikungi na Milioni 476 kwaajili ya Kituo cha Polisi Mkalama" Alisema Mhandisi Masauni.

 Mhandisi Masauni amesema ujenzi wa vituo vya  Polisi vya Mkalama na Ikungi utafanyika kwa awamu hivyo kufika kwake kwenye Wilaya hizo ni Utekelezaji wa Maagizo ya Katibu Mkuu Chongolo pamoja na kuangalia namna nzuri ya kumalizia ujenzi huo.

Aidha Mhandisi Masauni Amewatoa hofu Askari Polisi kuhusu miundombinu yao ambapo amemwakikishia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida kuwa hivi karibuni atarudi kufanya ziara ya kukagua miundombinu ya jeshi hilo la Polisi.

"Niwatoe hofu askari pamoja na wananchi tunajua mazingira bado sio rafiki lakini kwa kuwa tumeshaanza kulifanyia kazi na kwamba ujenzi utakamilika katika muda uliopangwa"aliongeza Mhandisi Masauni.

Amesema katika bajeti iliyopita serikali imezindua mpango wa kujenga nyumba na ofisi za Askari Polisi ikiwemo vya Mkalama na Ikungi hapa Singida vikiwa ni miongoni mwa vituo ambavyo vilikuwa havijakamilika.

Ujenzi wa Kituo cha Polisi Mkalama ulianza Mwaka 2015 na kufikia 2016 ujenzi ukasimama kutokana na kuisha kwa fedha za ujenzi huyo ambapo hadi Kukamilika kwake utatumia shilingi Milioni 567,148,000/=

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Daniel Chongolo alitoa agizo la kumaliziwa kwa ujenzi wa vituo hivyo wakati wa ziara yake ya  kuimarisha chama cha Mapinduzi na kukagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020 - 2025 kwa Mkoa wa Singida Ziara iliofanyika Februari 27 hadi Machi 4 2023.


No comments:

Post a Comment