Rai hiyo
imetolewa jijini dodoma na mkuu wa wilaya ya Bahi Mhe.MWANAHAMISI MUNKUNDA
kwenye kongamano la wanawake wa kiislamu lilofanyika jijini Dodoma masjid
ghadaf lenye lengo la kuukuza uislamu na ujenzi bora wa akhera kwa waislam
liloandaliwa na Taasisi ya Jamiiyatul
Akhlaaqul Islaam JAI Dodoma.
Aidha MWANAHAMISI
MUNKUNDA amesema serikali itaendelea kushirikiana na taasisi hiyo ya JAI ili kuirahisishia
taasisi hiyo ya JAI kuweza kutekeleza majukumu yake ya kutoa huduma mbalimbali
katika jamii.
Kwa upande
wake mbunge wa viti maalum Mkoa wa Dodoma Mhe. FATMA TOUFIQ akatumia fursa hiyo
kuwataka wanawake wa kiislam hususani kinamama kuhakikisha wanawalea watoto wao
katika maadili yaliyo mema ikiwemo kuwasomesha elimu ya dini pamoja na
kuhakikisha mabinti wa kiislam wanavaa mavazi yenye stara.
Naye Sheikh wa
mkoa wa Dodoma Alhaj MUSTAFA RAJABU akawataka wanawake wakiislam kuhakikisha
wanawaongoza mabinti wao katika kutenda matendo mema na kufata tabia nzuri za
uislam na kuachana na tabia ambazo sio za kiislam.
Pia Sheikh MUSTAFA
RAJABU akatumia fursa hiyo ya kongamano liloandaliwa na Taasisi ya JAI Dodoma
kuishukuru Taasisi hiyo ya JAI kutokana na misaada mbalimbali inayotoa katika
jamii ikiwemo kuwahudumia wagonjwa na utoaji wa damu kwa watu wenye uhitaji.
Amir wa Taasisi ya Jamiiyatul Akhlaaqul Islaam JAI Dodoma Sheikh ALLY KANDA akitoa salam za Taasisi hiyo ya JAI Dodoma amesema kazi za Taasisi hiyo ni kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji katika jamii huku Mweka Hazina Msadizi wa Taasisi hiyo ya JAI Dodoma Ukhut ASIA MUHAMMED akisoma Risala kwa mgeni rasmi ameeleza malengo ya kuanzishwa kwa Taasisi hiyo ikiwemo kuchangia damu kwa watu wenye uhitaji na kuwahudumia wagonjwa hospitalini.
No comments:
Post a Comment