Thursday, June 20, 2019

MHE.MGALU AWASHA UMEME VIJIJI VYA BICHA,KOLO NA KWAYONDU KONDOA MKOANI DODOMA

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa kata ya Kilimani wilayani Kondoa kabla ya kuwasha umeme katika Shule ya Sekondari Bicha.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akikata utepe kuashiria umeme kufika kwenye Shule ya Sekondari ya Bicha wilayani Kondoa.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwasha umeme katika Shule ya Sekondari ya Bicha iliyopo kata ya Kilimani wilayani Kondoa.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne katika Shule ya Sekondari ya Bicha mara baada ya kuwasha umeme.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akicheza na wananchi wa kijiji cha Kolo mara baada ya kuwasili kuwasha umeme katika Zahanati ya Kolo wilayani Kondoa.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi katika Zahanati ya Kolo wilayani Kondoa kabla ya kuwasha umeme katika zahanati hiyo.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akikata utepe kuashiria umeme kufika kwenye Zahanati ya Kolo wilayani Kondoa Mkoani Dodoma.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwasha umeme katika Zahanati ya Kolo iliyopo wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi katika Kijiji cha  Kwayondu wilayani Kondoa huku akiwa ameshika kifaa cha umeme Tayari (UMETA) akiwapa elimu ya kutumia umeme huo kabla ya kuwasha umeme katika Kijiji hicho.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizindua umeme kuashiria kufika katika kijiji cha Kwayondu wilayani Kondoa Mkoani Dodoma.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwasha umeme katika shule ya Sekondari ya Kwayondu iliyopo kijiji cha Kwayondu wilayani Kondoa Mkoani Dodoma.


………………….

Na.Alex Mathias,Kondoa

Naibu Waziri wa Nishati Mhe.Subira Mgalu  amefanya ziara ya kuwasha umeme katika wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma ambapo amewasha katika Shule ya Sekondari Bicha,Zahanati ya Kolo pamoja na kijiji cha Kwayondu  ikiwa ni juhudi za Serikali za kuhakikisha kila mwananchi aweze kuunganishiwa umeme.

Mhe.Mgalu amesema kuwa, kuwashwa kwa umeme katika vijiji hivi  ni muendelezo wa utekelezaji wa adhma ya Serikali ya Awamu ya Tano kufikisha umeme katika Vijiji vyote nchini.

Aidha Mgalu akizungumza na wananchi huku akitoa elimu kuhusu gharama za kuwaunganishia umeme amesema Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli inawajibu ya kuwajali na kuwathamini wananchi wa kipato cha chini.

Amesema kuwa Serikali imeamua kushusha gharama za kuwaunganishia umeme wananchi wake hadi shilingi 27,000/= tu.

“Hapo mwanzo gharama za kuunganishiwa umeme zilikuwa ni shilingi 177,000, lakini Serikali kwa vile inawajali wananchi wake imelipa shilingi 150,000/= kwa kila anayeweka umeme, na kazi ya mwananchi ni kulipia kiasi kidogo tu cha shilingi 27,000/=, tofauti na hapo awali.” amesema Mhe.Mgalu

Hata hivyo Mhe.Mgalu, pia amesisitiza wananchi kutumia vifaa vya Umeme Tayari (UMETA) ambavyo vitawawezesha kuondokana na gharama za wiring na kuwezesha kuunga wateja wengi .

“Gharama hizo za wiring zimeonekana kuwa ndio changamoto kwa wananchi na serikali imepokea changamoto hizo na kuwa itazifanyia kazi.” amesisitiza

Naibu Waziri huyo ameutaka  uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Dodoma na Kondoa kuhakikisha wanakamilisha usambazaji wa umeme kwa wanakijiji ili waweze kunufaika na huduma hiyo.

No comments:

Post a Comment