Wednesday, December 5, 2018

Jengo la Wizara ya Madini kukamilika ifikapo Januari 4, 2019


Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa pili kushoto) akiambatana  na Viongozi Waandamizi wa Wizara ya Madini mara baada ya kufika katika eneo la ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Madini eneo la Ihumwa jijini Dodoma.


Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa tatu) wakitoka kukagua eneo la ujenzi wa jengo la Wizara.


Muonekano wa moja wapo wa jiwe lililopo katika eneo la kujenga Jengo la Wizara ya Madini.

Na Rhoda James – Dodoma

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ameagiza Kampuni ya Mzinga Holding Co. Ltd kukamilisha ujenzi wa Jengo la Wizara ya Madini ifikapo Januari 4 mwaka 2019.

Ametoa agizo hilo jana tarehe 4 Desemba, 2018 alipofanya ziara ya kukagua eneo la ujenzi wa ofisi za Wizara lililopo Ihumwa Jijini Dodoma akiambatana na viongozi wengine waandamizi wa wizara.

Kairuki alibainisha kuwa baada ya sikukuu za mwisho wa mwaka, viongozi wote watatakiwa kuhamia katika eneo hilo kutokana na ukweli kuwa ifikapo Januari 4 jengo hilo litakuwa limekamilika.

Aidha, Waziri Kairuki ameshauri kuwa wakati wanaendelea na maandalizi mengine waendelee na manunuzi ya vifaa, na vifaa hivyo lazima viwe vya viwango ikiwezekana watumie dealers ambao ni wakubwa na wa uhakika.

Kwa upande wake, Mhasibu Mkuu wa Wizara, Anthony Tarimo alisema kuwa pesa kwa ajili ya ujenzi huo ipo, wao wanachohitaji ni kujua mkataba ukoje na guarantee ili pesa kwa ajili ya ujenzi huo itolewe.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Issa Nchasi ameeleza kuwa wamejiandaa kikamilifu ili kusimamia ujenzi wa Jengo hilo na atateua watu ambao watafutilia kwa ukaribu shughuli za kila siku za ujenzi wa Jengo hilo.

Vile vile, Mwakilishi wa Kampuni ya Mzinga Holding Co. Ltd, Mhandisi Hagai Mziray amesema wataanza maandalizi ya ujenzi wa Jengo la Madini mapema tarehe 5 Decemba, 2018 na watafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kuwa wanakamilisha ujenzi kwa wakati.

Mziray ameongeza kuwa Kampuni yao inao uzoefu wa kutosha katika masuala ya ujenzi kwani wamejihusisha na ujenzi wa majengo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Manispa ya jiji Dodoma, Hosipitali ya Makole, Hosipital ya Mkoa wa Morogoro pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi.

Kwa sasa Wizara ya Madini inatumia Ofisi za Wakala wa Jiologia Tanzania (GST) zilizopo Mjini Dodoma.
Captions
Pic 1
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa pili kushoto) akiambatana  na Viongozi Waandamizi wa Wizara ya Madini mara baada ya kufika katika eneo la ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Madini eneo la Ihumwa jijini Dodoma.
Pic 2
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa kwanza) akiondoka eneo la ujenzi wa Jengo la Madini mara baada ya kukagua eneo hilo ambalo linakhadiriwa kuwa na hekta 3-4.
Pic 3
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa pili kulia) akijadili jambo na Manaibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia) na Stanslaus Nyongo (wa tatu kulia) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Saimon Msajila (kushoto) wengine katika picha ni Viongozi mbalimbali wa wizara.
Pic 4, 5 na 6
Muonekano wa eneo la ujenzi wa Jengo la Wizara ya Madini. 
Pic 7
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa tatu) wakitoka kukagua eneo la ujenzi wa jengo la Wizara.
Pic 8
Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na rasilimali watu Nsajigwa Kabigi, akitoa maelezo kwa Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (katikati) kuhusu eneo la ujezi wa Ofisi ya Madini.
Pic 9
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki akijadili jambo na Mhasibu Mkuu wa Wizara, Anthony Tarimo (wa pili) wakati walipokuwa wakikagua eneo la ujenzi wa Jengo wa Wizara tarehe 4 Decemba, 2018.
Pic 10
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa tatu) akiwa na Viongozi Waandamizi wakati wa ukaguzi wa eneo la ujezi wa Jengo la Madini tarehe 4 Decemba, 2018.
Pic 11
Muonekano wa moja wapo wa jiwe lililopo katika eneo la kujenga Jengo la Wizara ya Madini. 




No comments:

Post a Comment