Friday, May 11, 2018

MHE BITEKO AITAJA WILAYA YA BUKOMBE KUWA YA PILI KWA MTANDAO WA BARABARA MKOANI GEITA

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko (Mb) ambaye ni Naibu Waziri wa Madini akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe kwenye kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi. Picha Zote Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko (Mb) ambaye ni Naibu Waziri wa Madini akisisitiza jambo kwenye kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani humo.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko (Mb) ambaye ni Naibu Waziri wa Madini akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe kwenye kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi.

Na Mathias Canal, Bukombe-Geita

Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita inaongoza kwa mtandao wa barabara ambapo jumla ya kilomita 1346 zinakutikana katika mtandao huo.

Hayo yamebainishwa leo 11 Mei 2018 na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko (Mb) ambaye ni Naibu Waziri wa Madini wakati akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe kwenye kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi uliopo katika eneo la kitongoji cha Uhamiaji, Kata ya Ketente.

Amesema kuwa Wilaya hiyo ni ya pili ikiwa nyuma ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambayo ndiyo inaongoza Mkoani Geita kwa kuwa na mtandao wa barabara ambazo zina urefu wa kilomita 1500.

Aidha, alisisitiza kuwa tayari barabara mpya zimefunguliwa katika kila eneo Wilayani Geita ambapo pia maombi maalumu yametumwa kwa ajili ya kurekebisha barabara zote zinazoharibika hivyo kuwaomba wananchi kushauri na kutunza kwa ufasaha barabara zote.

Akizungumzia kuhusu sekta ya elimu Mhe Biteko amewaeleza wajumbe hao wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe kuwa tayari serikali imeongeza shule za sekondari Businda kuwa na kidato cha tano na sita hivyo kuwa na shule mbili ikiwemo shule ya Sekondari Runzewe.

Alisema kuwa ongezeko la shule hiyo litapelekea wanafunzi kupata elimu ya ngazi ya kidato cha tano na cha sita kwa urahisi tofauti na changamoto iliyokuwepo awali kwani wamekuwa wakitumia umbali mrefu kutafuta elimu.

Sambamba na hayo alisema kuwa jumla ya shilingi milioni 440 zinahitajika kwa ajili ya upanuzi wa mabweni ili kurahisisha huduma za malazi kwa wanafunzi wilayani humo.

Katika hatua nyingine Mbunge huyo ametafu Computer kwa ajili ya shule hizo mbili ambapo msaada huo ameipata kutoka kampuni ya Vodacom na Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi.

Kuhusu Mikopo kwa makundi mbalimbali, Wilaya ya Bukombe inaongoza kwa kuwa nafasi ya kwanza Mkoani Geita kwa kupata fedha hizo za mikopo jumla ya shilingi milioni 541 ambazo zimetolewa katika awamu tatu.

Mhe Biteko aliwaomba wajumbe hao wa Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Wilayani Bukombe kutoendeleza makundi yaliyojitokeza wakati wa kampeni badala yake kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa ajili ya utekelezaji wa ilani ya ushindi wa chama hicho ya mwaka 2015-2020.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment