Sunday, January 14, 2018

DKT ANGELINE MABULA AWATAKA WANANCHI KUWA WAZALENDO





Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambae pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Dkt Angeline Mabula amewataka wananchi kuwa wazalendo kwa kuwafichua wasio raia wa Tanzania katika zoezi la uandikishaji vitambulisho vya Taifa.

Mhe Dkt Angeline Mabula ameyasema hayo alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha uandikishaji wa vitambulisho vya taifa (NIDA) kilichopo ofisi ya kata ya Ibungilo ambapo amewaasa wananchi waliokuwa wamepanga foleni kwaajili ya zoezi hilo kuwa makini na waangalifu katika ujazaji wa fomu za maombi sanjari na kuwaripoti wale wote wasiostahili wakitaka kutumia mwanya huo kujipatia vitambulisho hivyo huku akiwaelimisha juu ya  umuhimu wa kuwa na kitambulisho hicho

‘… Lazima muwe makini mnapojaza taarifa zenu lakini lingine sisi ni wa Tanzania tunatakiwa kuwa wazalendo kama unajirani yako ambaye si Mtanzania na amepanga foleni kutaka kupata kitambulisho cha taifa toa taarifa mapema, Tusiwape watu wasiohusika  ni nyinyi wakuisaidia Serikali vinginevyo vitambulisho vyetu vitachukuliwa na watu wasiokuwa waTanzania …’ Alisema

Kwa upande wake msimamizi wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa  (NIDA)  kata ya Ibungilo Ndugu Eric Elisha mbali na kueleza juu ya mwenendo wa zoezi hilo kwa kata anayoisimamia amemuhakikishia mbunge huyo umakini na uzingatiaji wa haki kuhakikisha kila mwananchi anayestahili anapata kitambulisho

Nao wananchi waliojitokeza katika zoezi la uandikishaji wamemshukuru Mhe Mbunge kwa kufanya ziara hiyo ya kushtukiza kukagua mwenendo wa zoezi huku wakiwasilisha changamoto wanazokutana nazo na kumuomba kuwasaidia namna ya kuzipatia ufumbuzi

Ziara hiyo ya gafla pia ilihusisha kulitembelea na kuzungumza na wafanya biashara wa soko kuu la wilaya hiyo la  Kiloleli kujua changamoto wanazokutana nazo ili kuzipatia ufumbuzi huku akiwaasa wale wote wanaofanya biashara nje ya soko kurudi sokoni hapo kwani nafasi bado zipo zakutosha
‘ Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga’

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge 
Jimbo la Ilemela 


14.01.2018

No comments:

Post a Comment