Waziri
wa nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za
mitaa(TAMISEMI)mhe. Selemani Jafo amewaagiza viongozi wa kampuni ya
UDART kufanya kila wawezalo ili ifikapo alhamisi ya wiki ijayo ili
kurudisha huduma ya mabasi ya mwendokasi kama ilivyokuwa awali.
Jafo
ametoa kauli hiyo leo alipotembelea maeneo tofauti ya huduma ya mabasi
ya mwendokasi jijini Dar es salaam na kujionea uharibifu mkubwa wa
baadhi ya magari ya mwendokasi uliosababishwa na mafuriko yaliyotokea
wiki hii jijini humo.
Katika
ziara hiyo, Jafo ameanzia katika kituo cha mabasi cha Kivukoni, na
kukagua eneo la Jangwani na kuishia kumalizia ziara yake hiyo katika
kituo cha Gerezani.
Akiwa
katika kituo cha Jangwani amebaini uharibifu mkubwa wa zaidi ya mabasi
35 ambayo yameingia maji na kuharibika kwa baadhi ya vipuri ambavyo
tayari vimeshaagizwa kutoka Dubai na vinatarajiwa kuingia nchini kuanzia
jumanne.
Amesema endapo vifaa hivyo vikifika nchini vitachukua kutwa moja kuvifunga kwa mabasi yote yaliyopata madhara.
Kufuatia
hali hiyo, Jafo ameagiza magari hayo ya mwendo kasi kuhamishiwa kwa
muda eneo la wazi la Gerezani linalomilikiwa na DART ili kuepusha
uharibifu mkubwa wa mabasi hayo endapo mvua zitaendelea kunyesha kwani
kwa hali ya sasa eneo la Jangwani sio rafiki kwa kipindi hiki cha mvua.
Jafo
amewaagiza DART kuwasiliana na jeshi la polisi jijini humo kuweka
utaratibu mzuri katika mataa ili mabasi ambayo hayajapata madhara yaweze
kutembea kwa mpangilio mzuri ili kusaidia wasafiri wasikwame vituoni
kwa muda mrefu wakati huu ambao magari mengine yanafanyiwa matengenezo
ya haraka.
Aidha
amemuagiza mtendaji mkuu anaye simamia mradi wa Dar es salaam
Metropolitan Development Project ( DMDP ) kuwasiliana na DAWASA ili
wafanye kikao cha haraka waangalie jambo la haraka la kufanya ili
kusafisha eneo la chini la mto Msimbazi ili kuondoa tope lililo ziba
mifereji ya kupitisha maji kitendo kinacho sababisha maji kusambaa eneo
lote la Msimbazi mvua zinaponyesha.
Kadhalika,
alisema serikali ipo katika mpango kabambe wa kuliboresha bonde la
Msimbazi kupitia mradi wa DMDP unaofadhiliwa na benki ya dunia ambao
wataalam watakuja na namna bora ya kulijenga bonde la Msimbazi ili
liweze kupitisha maji yote na kuyapeleka baharini.
No comments:
Post a Comment