Waziri wa
Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwasili katika uwanja
mdogo wa Wasso Makao makuu ya wilaya ya Ngorongoro katika mji wa
Loliondo mapema leo Oktoba 26,2017.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwasili katika uwanja mdogo wa Wasso Makao makuu ya wilaya ya Ngorongoro katika mji wa Loliondo mapema leo Oktoba 26,2017.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwasili katika uwanja mdogo wa Wasso Makao makuu ya wilaya ya Ngorongoro katika mji wa Loliondo mapema leo Oktoba 26,2017.
Waziri wa
Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwasili katika uwanja
mdogo wa Wasso Makao makuu ya wilaya ya Ngorongoro katika mji wa
Loliondo mapema leo Oktoba 26,2017.
Na Mwandishi Wetu,
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla
amewasili Makao makuu ya Wilaya ya Ngorongoro na kisha kufanya mkutano maalum
na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo ambapo kisha atazungukia kwenye
maeneo yenye migogoro.
Waziri Dkt.Kigwangalla ametua uwanja mdogo wa Wasso uliopo
eneo la Loliondo na kisha kukutana na viongozi hao wa Ulinzi na Usalama
wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Rashid Mfaume Taka.
Dk Kigwangalla baada ya kumaliza kikao hicho maalum na wakuu
hao, anatarajia kutembelea maeneo yenye migogoro ili kubaini kiini cha mgogoro
wa eneo hilo la pori tengefu la Loliondo.
Aidha, pia anatarajia kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo
pamoja na kufanya mkutano wa wazi ikiwemo kusikiliza kero kutoka kwa wananchi
hao.
Waziri Dkt.Kigwangalla yupo Mkoani Arusha kwa ziara ya sita
ambapo awali alianza kutembelea Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA)mjini
Arusha, na baadae Mamlaa ya Hifadhi ya Ngorongoro ambapo pia aliweza kukutana
na jamii ya wafugaji wanaoishi kwenye hifadhi ya Ngorongoro kwa namna ya
kitatua migogoro kati yao na wahifadhi wa Ngorongoro.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment