METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, July 14, 2017

MKUU WA WILAYA YA UBUNGO MHE KISARE MAKORI AZUIA WAFANYABIASHARA KATIKA SOKO LA NDIZI MABIBO KUONDOLEWA BILA UTARATIBU MAALUMU

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza na wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakati wa ziara ya kikazi katika eneo hilo
Wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori wakati akizungumza nao alipotembelea katika eneo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori (Kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakati wa ziara ya kikazi katika soko la Ndizi-Mabibo
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori (Kulia) akiwasikiliza wananchi wakieleza kero zao wakati wa ziara ya kikazi katika soko la Ndizi-Mabibo. Mwingine ni Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ubungo Ndg Salum Kali
Wakuu wa Idara na Vitengo Manispaa ya Ubungo wakifatilia mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori uliofanyika katika Soko la Ndizi-Mabibo Jijini Dra es salaam
Wananchi pamoja na wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori wakati akizungumza nao alipotembelea katika eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori Leo Julai 14, 2017 amezuia utaratibu uliotaka kutumiwa na Uongozi wa Kiwanda cha Nguo cha Urafiki kilichopo katika Kata ya Mabibo wa kutaka kuwatoa wafanyabiashara katika soko la Ndizi-Mabibo Jijini Dar es salaam kwa madai ya kutaka kujenga Ukuta kwa ajili ya kiwanda hicho.

Mhe Makori alisema kuwa Kauli za tishio la kujengwa ukuta na kuwaondoa wafanyabiashara wote katika soko hilo alizipata jana mchana (13/7/2017) na kuamua kufanya mkutano na wananchi sambamba na wafanyabiasha katika soko hilo.

Mkuu wa Wilaya ya ubungo Mhe Makori amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo ndg john lipesi Kayombo kutotoa kibali cha ujenzi wa ukuta unaotaka kujengwa na Uongozi wa Kiwanda cha nguo cha Urafiki mpaka pale watakapofuata utaratibu.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli imeagiza kuwaondoa wafanyabiashara hususani machinga endapo tu kama kuna maeneo ya kuwapeleka katika maeneo rafiki watakapofanya biashara kwa Amani pasina mashaka.

“Kwa kuwa wafanyabiashara hawa bado hatujaainisha eneo la kuwapeleka kwahiyo nakuagiza leo Mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha hawaondoki kwani wanalipa kodi kwa ufasaha hivyo sihitaji wasumbuliwe na mtu yoyote” 

“Kama wafanyabiashara hawakwepi kodi kwanini kikundi kimoja cha wala rushwa ndicho kianze kutaka kuwagombanisha wananchi na kuichukia serikali yao kisa tu tumeziba mianya yao ya ulaji ” Alisema Mhe Makori

Mhe Makori alisema kuwa kuna kikundi cha wafanyabiashara katika soko hilo kinaitwa Majimoto ndicho ambacho kinachochea kadhia hiyo ya kuhamasisha uongozi wa kiwanda hicho kuanza chokochoko za kutaka kuwafukuza wafanyabiashara hao.

Sambamba na hayo pia Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo kuwaagiza wataalamu wa Mazingira ili kufatilia kiwanda hicho ambacho kinalalamikiwa na wananchi kuathiri afya zao kutokana na Moshi unaotoka kiwandani hapo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA MKUU WA WILAYA YA UBUNGO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com